UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
UNIVERSITY HEALTH CENTRE (UHC)

Vyakula kwa Mgonjwa Mwenye Kisukari

Vyakula Vyenye Wanga: Vyakula hivi ni pamoja na aina zote za nafaka, viazi aina zote mihogo, magimbi, na Ndizi. Vyakula hivi huupatia mwili nguvu.

 

Vyakula Vyenye Protini: Aina hii ya vyakula ni pamoja na maharage, kunde, mbaazi, soya, karanga, njegere, njugu mawe, dengu, choroko, asili ya wanyama ni: nyama, mayai, samaki, dagaa, kumbikumbi, senene, maziwa na nzige. Vyakula hivi hujenga mwili.

 

Vyakula Vyenye Vitamini na Madini: Aina hizi za vyakula ni pamoja na matunda aina zote na mboga-mboga za aina mbalimbali. Vyakula hivi huupa mwili kinga imara dhidi ya maradhi mbalimbali

 

Vyakula Vyenye Mafuta na Sukari: Aina hii ya vyakula ni pamoja na mafuta ya kupikia, aina zote za ufuta asali, miwa nakadhalika.

 

Tafadhali bonyeza hapo chini kupakua jarida kwa maelezo zaidi

Attachment: Download