UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
UDSM HOSPITAL (UH)

Madhara ya Dawa za Kulevya

Dawa za kulevya ni kemikali ambazo ziingiapo mwilini huathiri ubongo wa mtumiaji na kumsababishia kuwa na matendo, hisia, fikra na muonekano tofauti na matarajio ya jamii.

 

Kemikali hizi hutokana na mimea na madini ambayo ni mali ghafi muhimu kwa mahitaji mengine ya mwanadamu. Dawa hizi huingia mwilini kwa njia kuu tatu:

  • Njia ya kunywa / kula
  • Kuvuta na
  • Kujidunga sindano

 

Dawa za kulevya ziko ambazo zimeruhusiwa kisheria kama tumbaku na pombe; ambazo hazijaruhusiwa kama bangi, mirungi, cocaine, heroin na mandrax; na zinazoruhusiwa kwa matumizi ya hospitali kama Valium, pethedine, morphine n.k

 

Tafadhali bonyeza hapo chini kupakua jarida kwa maelezo zaidi

Attachment: Download